NATIONWIDE HIT SINGLES BY MNYALU
Msanii huyu ambaye jina lake halisi ni Mike Mwakatundu toka Nyaluland ambaye anachukua Diploma ya Biashara katika chuo cha biashara CBE mjini Dar es salaam,.
Kijana huyu mahiri na mwenye kutabasam muda wote toka viwanja vya Nyaluland (nyanda za juu kusini) Mkoani Iringa, alivamia ofisi za Darhotwire kwa kishindo akiwa ameongozana na mshikaji wake ambaye alishiriki katika kibao chake cha Tamati aitwaye Adili a.k.a 'Hisabati' ambaye pia anavurumisha ubeti wa kwanza wa wimbo wa mkali Profesa J uitwao nawakilisha.
Siku ya tarehe 15 April 05 Mike Tee alisema haya kwa Muandishi wetu -
Muandishi : Mike Tee mambo vipi? na pia karibu sana,
Mike Tee: mambo yangu ni shwari na aksante sana kwa kunipokea japo tubadilishane mwawili matatu,
Muandishi : Naona watu wanakuelewa wanakubali kazi yako na labda ni nini siri ya mafanikio yako
Mike Tee: Ndugu yangu siwezi kujua ni nini hasa kwanini watu wanakubali kazi yangu unajua inakuwa kama miujiza kwa jinsi nilivyoanza na sasa karibu east africa najulikana na wengi wananisifu kazi yangu ni nzuri ukweli siwezi jua ni nini hasa
CONTINUES
|